1 Samweli 19:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
9 Halafu, pepo muchafu kutoka kwa Yawe akamushika Saulo alipokuwa akiikaa ndani ya nyumba yake, akishika mukuki katika mukono, wakati Daudi alikuwa akipiga kinubi.
Yawe akamwuliza: ‘Kwa namna gani?’ Naye akajibu: ‘Nitakwenda na kuwasukuma manabii wake wote waseme uongo.’ Yawe akamwambia: ‘Wewe utamushawishi na utashinda; basi, kwenda ufanye hivyo.’
Sasa, ee bwana wetu, amuru watumishi wako wanaokutumikia wamutafute mutu mwenye ufundi wa kupiga kinubi, na huyo pepo muchafu kutoka kwa Mungu atakapokufikia, mutu yule atapiga kinubi, nawe utapata utulivu.”
Kisha kulikuwa vita tena kati ya Wafilistini na Waisraeli. Daudi alitoka akapigana na Wafilistini, akawaua Wafilistini wengi na waliobaki wakamukimbia.
Siku moja, Saulo alikuwa Gibea, akiikaa chini ya muti wa mukwaju, kwenye mulima, naye alikuwa na mukuki wake katika mukono na watumishi wake walikuwa wakimuzunguka. Basi akaambiwa kwamba Daudi na watu wake wameonekana.