Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 19:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Kisha kulikuwa vita tena kati ya Wafilistini na Waisraeli. Daudi alitoka akapigana na Wafilistini, akawaua Wafilistini wengi na waliobaki wakamukimbia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 19:8
8 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, mufalme wa Israeli akashinda vita, akateka farasi na magari ya vita mengi, na kuwaua Waaramu kwa wingi.


Hata jeshi likinizunguka, moyo wangu hautaogopa kitu; hata nikishambuliwa kwa vita, sitakata tumaini.


Daudi alifanikiwa katika kila kitu alichofanya, maana Yawe alikuwa pamoja naye.


Waaskari wa Wafilistini walikwenda kupigana na Waisraeli, lakini kila mara walipopigana vita, Daudi alipata ushindi kuliko watumishi wa Saulo. Hivyo jina la Daudi likazidi kusifiwa sana.


Hivyo, Yonatani akamwita Daudi na kumwelezea mambo hayo yote. Yonatani akamupeleka Daudi kwa Saulo, na Daudi akamutumikia Saulo kama hapo zamani.


Halafu, pepo muchafu kutoka kwa Yawe akamushika Saulo alipokuwa akiikaa ndani ya nyumba yake, akishika mukuki katika mukono, wakati Daudi alikuwa akipiga kinubi.


Basi, Daudi akaenda Keila pamoja na watu wake, na kule akapigana na Wafilistini, akawaua Wafilistini wengi na kunyanganya ngombe wengi. Kwa hiyo Daudi aliwaokoa wakaaji wa Keila.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ