1 Samweli 19:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
24 Alivua nguo zake, akatabiri mbele ya Samweli. Alibaki uchi kwa siku moja, muchana na usiku. Kwa hiyo watu walianza kujiuliza: “Hata Saulo ni mumoja wa manabii?”
Daudi aliporudi kwake kwa kuibariki jamaa yake, Mikali, binti ya Saulo, alikwenda kumupokea, akasema: “Ni ajabu kwa mufalme wa Waisraeli kujiheshimu leo, kwa kujifunua uchi wake mbele ya watumishi wake na wajakazi wake sawa vile mushenzi anavyovua nguo zake mbele ya watu bila haya!”
Miaka mitatu mbele ya pale, Yawe alimwambia Isaya mwana wa Amozi hivi: Kwenda uvue nguo ya gunia uliyokuwa umevaa katika kiuno, na viatu vyako. Isaya akafanya kama alivyoambiwa; akakuwa anatembea uchi na bila viatu.
Wote waliomusikia walishangaa, wakisema: “Si mutu huyu ndiye aliyewatesa vikali kule Yerusalema watu wanaoomba kwa jina la Yesu? Hakika amefika huku nako kusudi awafunge watu kama hao na kuwapeleka kwa wakubwa wa makuhani.”
Tangu siku ile, Samweli hakumwona tena Saulo, mpaka siku alipokufa. Hata hivyo Samweli alimulilia Saulo. Naye Yawe alisikitika kwamba alikuwa amemusimika Saulo kuwa mufalme juu ya inchi ya Israeli.
Kesho yake, pepo muchafu kutoka kwa Mungu akamushambulia Saulo kwa rafla, akakuwa anapayukapayuka kama mwenda-wazimu katika nyumba yake. Daudi alikuwa anapiga kinubi kama alivyofanya siku zote. Saulo alikuwa na mukuki katika mukono wake.