Daudi alipotoroka, alikwenda Rama kwa Samweli. Alimwelezea Samweli mambo yote aliyomufanyia Saulo. Basi, Daudi na Samweli walikwenda na kukaa kule Nayoti.
Kwa hiyo Saulo akatuma watu kwenda kumukamata. Lakini walipokuta kundi la manabii likitabiri na Samweli akiliongoza, Roho wa Mungu aliwafikia wale watumishi wa Saulo, nao vilevile wakaanza kutabiri.
Saulo alipokuwa angali kule Gibea, Wazifu wakamwendea na kumwambia: “Daudi anajificha katika inchi yetu kwenye makimbilio kule Horeshi, kwenye mulima Hakila, unaokuwa upande wa kusini wa jangwa.
Wamoja kati ya wanaume kutoka muji wa Zifu wakamwendea Saulo kule Gibea, wakamwambia kwamba Daudi alikuwa anajificha kwenye mulima Hakila, upande wa mashariki wa Yesimoni.