1 Samweli 19:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
18 Daudi alipotoroka, alikwenda Rama kwa Samweli. Alimwelezea Samweli mambo yote aliyomufanyia Saulo. Basi, Daudi na Samweli walikwenda na kukaa kule Nayoti.
Kesho yake asubui, Elekana na jamaa yake waliamuka asubui mapema, na kisha kumwabudu Yawe, walirudi kwao Rama. Elekana akalala na muke wake Hana na Yawe akamukumbuka.
Kwa hiyo yeye mwenyewe akaenda Rama. Alipofika kwenye kisima kikubwa kinachokuwa kule Seku, akamukuta mutu fulani ambaye alimwuliza: “Samweli na Daudi wako wapi?” Yule mutu akamujibu: “Wako Nayoti, katika muji wa Rama.”
Naye Saulo akaenda kule Nayoti katika muji wa Rama. Alipofika kule, Roho wa Mungu akamufikia, naye alianza kutabiri akiwa katika njia mpaka alipofika Nayoti katika muji wa Rama.
Daudi alikimbia kutoka Nayoti katika Rama, akaenda mpaka kwa Yonatani, akamwambia: “Nimefanya nini? Kosa langu ni gani? Nimemutendea baba yako zambi gani hata anajaribu kuyaangamiza maisha yangu?”
Wakati ule, Samweli alikuwa amekwisha kufa, na Waisraeli wote walikuwa wamekwisha kumwombolezea na kumuzika katika muji wake Rama. Saulo alikuwa amewafukuza kutoka katika inchi wenye kutabiri na wachawi.