Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 19:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Halafu Saulo akamwuliza Mikali: “Kwa nini umenidanganya? Umemwacha adui yangu atoroke?” Naye Mikali akamujibu Saulo: “Aliniambia: ‘Uniache niende kusudi nisipate kukuua.’ ”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 19:17
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Watumishi wa Abusaloma walipofika kwa yule mwanamuke, wakamwambia: “Ahimasi na Yonatani wako wapi?” Yule mwanamuke akawaambia: “Wamekwenda ngambo ya kijito.” Walipowatafuta na kuwakosa, wakarudi Yerusalema.


Abeneri akamwambia Asaeli mara ya pili: “Acha kunifuatilia. Kwa nini nikuue? Nitaweza kuonana na kaka yako Yoabu?”


Basi, Ahabu alipomwona Elia, akasema: “Ewe adui yangu, umeninasa tena?” Elia akamujibu: “Ndiyo! Nimekunasa, kwa sababu wewe umekusudia kabisa kutenda maovu mbele ya Yawe.


Herode alipoona kwamba wale watu wenye elimu wamemudanganya, akakasirika sana. Akatuma watu Betelehemu na popote kandokando yake kwa kuua watoto wote waliokuwa na umri wa miaka miwili na chini yake. Alifanya vile kufuatana na jinsi alivyohakikishwa na wale wenye elimu juu ya wakati nyota ilipotokea.


Basi nimegeuka sasa adui yenu kwa sababu ya kuwaambia ukweli?


Saulo alipotuma watu kwa kumukamata Daudi, Mikali akawaambia kwamba Daudi ni mugonjwa.


Wale watu walipoingia ndani ya nyumba ya Daudi na kukiangalia kitanda, waliona kuna sanamu na kiegemeo cha manyoya ya mbuzi kwenye kichwa.


Saulo akawaambia walinzi waliokuwa wakisimama pembeni yake: “Mugeuke na kuwaua makuhani wa Yawe, maana wao wanapatana na Daudi; walijua kwamba ametukimbia wala hawakuniarifu.” Lakini walinzi hao hawakuinua mikono yao kwa kuwaua makuhani wa Yawe.


Yule mwanamuke alipomwona Samweli akalalamika kwa sauti kubwa, akamwambia Saulo: “Kwa nini umenidanganya? Wewe ni Saulo!”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ