12 Kwa hiyo Mikali akamutelemusha Daudi kupitia katika dirisha, naye akatoka na kutoroka.
Watumishi wa Abusaloma walipofika kwa yule mwanamuke, wakamwambia: “Ahimasi na Yonatani wako wapi?” Yule mwanamuke akawaambia: “Wamekwenda ngambo ya kijito.” Walipowatafuta na kuwakosa, wakarudi Yerusalema.
Yawe ni karibu na wenye kuvunjika moyo; anawaokoa wote waliokata tamaa kabisa.
Basi, Rahabu akawashusha hao watu kwa kamba kupitia katika dirisha: nyumba yake ilikuwa imejengwa ikiambatana na ukuta wa muji wa Yeriko.
Wana wa Saulo walikuwa: Yonatani, Iswi na Malkisua. Wabinti zake walikuwa wawili; muzaliwa wa kwanza aliitwa Merabu na mudogo aliitwa Mikali.