Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 19:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Saulo alijaribu kumuchoma Daudi kwa mukuki ule. Lakini Daudi aliepa mukuki wa Saulo na mukuki ukapiga ukuta. Daudi akakimbia na kutoroka.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 19:10
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Tumeponyoka kama ndege katika mutego; mutego umefyatuka, nasi tukaponyoka.


Mungu alinyoosha mukono wake kutoka juu, akanitwaa, alininyanyua kutoka ndani ya maji mengi.


Yawe ni karibu na wenye kuvunjika moyo; anawaokoa wote waliokata tamaa kabisa.


Mutu mwovu anamuvizia mutu wa haki, na kujaribu kumwua;


Maana wao wako mbio kutenda maovu, haraka zao zote ni za kumwanga damu.


Hakuna hekima, ufahamu, wala shauri yoyote ya mutu, itakayoweza kupingana na Yawe.


Silaha zote zilizotengenezwa kwa kukuzuru wewe hazitafaa kwa kitu chochote. Mutu akikushitaki, utamushinda. Hiyo ndiyo haki niliyowapangia watumishi wangu. Hizo ndizo haki nilizowahakikishia. –Ni ujumbe wa Yawe.


Lakini Yawe anasema hivi: Nitakutendea nini, ee Efuraimu? Nikufanyie nini, ee Yuda? Upendo wenu kwangu ni kama ukungu wa asubui, kama umande unaotoweka upesi.


Watakapowatesa katika muji mumoja, mukimbilie katika muji mwingine. Kweli ninawaambia: hamutamaliza kuzunguka katika miji yote ya Israeli mbele ya kurudi kwa Mwana wa Mutu.


Lakini yeye akapita katikati yao, na kujiendea.


Wakajaribu tena kumufunga Yesu, lakini akawaponyoka.


walizimisha moto mukali, waliponyoka kuuawa kwa upanga. Walikuwa wazaifu, lakini wakapata nguvu; walikuwa shujaa katika vita na kushinda majeshi ya kigeni.


Kesho yake, pepo muchafu kutoka kwa Mungu akamushambulia Saulo kwa rafla, akakuwa anapayukapayuka kama mwenda-wazimu katika nyumba yake. Daudi alikuwa anapiga kinubi kama alivyofanya siku zote. Saulo alikuwa na mukuki katika mukono wake.


Basi, alimutupia Daudi mukuki mara mbili maana alifikiri: “Nitamubanisha Daudi kwenye ukuta.” Lakini Daudi aliepa mara zote mbili.


Saulo alimusikiliza Yonatani, kisha akaapa: “Kama vile Yawe anavyoishi, sitamwua Daudi.”


Lakini Saulo akamutupia Yonatani mikuki kusudi amwue. Naye Yonatani akatambua kwamba baba yake alikuwa amekusudia kumwua Daudi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ