Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 18:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Waaskari walipokuwa wanarudi kwenye nyumba, pamoja na Daudi kisha kumwua yule Mufilistini, wanawake kutoka kila muji katika Israeli walitoka kwenda kumupokea mufalme Saulo. Wanawake nao walikuwa wanaimba nyimbo za furaha, wakipiga matari na vinubi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 18:6
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Musiuambie muji wa Gati jambo lile wala katika barabara za Askeloni, kusudi wanawake wa Wafilistini wasishangilie, wabinti za wapagani wasifurahi.


Daudi na watu wote wa Israeli, walikuwa wanaimba nyimbo na kucheza kwa nguvu zao zote, mbele ya Yawe. Walipiga ala za muziki zilizotengenezwa na muti wa muvinje: vinubi, vinanda, matari, kayamba na matoazi.


Mulisifu jina lake mukicheza, mumwimbie kwa ngoma na zeze.


Watu wako wakapata makao ndani yake, uliyotayarishia wamasikini kwa uzuri wako.


Ee Mungu, maandamano yako ya ushindi yanaonekana; maandamano ya Mungu wangu, mufalme wangu, katika pahali patakatifu!


Basi nabii Miriamu, dada ya Haruni, akatwaa ngoma katika mukono, na wanawake wengine wote wakamufuata wakiwa na ngoma zao ndogo wakicheza.


Miriamu akawaongoza kwa kuimba: “Mumwimbie Yawe maana ameshinda kwa utukufu. Farasi na mupanda-farasi wake amewatupa ndani ya bahari.”


Kila pigo la azabu ya Yawe juu ya Waasuria litaandamana na mudundo wa ngoma na zeze. Yeye mwenyewe atapigana na Waasuria.


Yefuta alipokuwa anarudi kwake kule Misipa, binti yake akatoka kuja kumupokea akicheza na kupiga matari. Binti huyo alikuwa ndiye mutoto wake wa pekee. Yefuta hakukuwa na mutoto mwingine mwanaume wala mwanamuke.


Kokote Daudi alikotumwa na Saulo, Daudi alifanikiwa. Hivyo, Saulo akamufanya kuwa mukubwa wa waaskari wake. Jambo hilo liliwafurahisha watu wote hata watumishi wa Saulo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ