Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 18:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Kwa sababu Yonatani alimupenda Daudi kama roho yake, alifanya agano naye.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 18:3
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mufalme alimwacha Mefiboseti mwana wa Yonatani kwa sababu ya kiapo ambacho Daudi na Yonatani mwana wa Saulo walikuwa wamefanya kati yao kwa jina la Yawe.


Warafiki wengi wanaweza kumwangusha mutu, lakini kuna rafiki mwaminifu kuliko ndugu.


Saulo alimwelezea mwana wake Yonatani na wakubwa wake juu ya mupango wake wa kumwua Daudi. Lakini Yonatani, mwana wa Saulo, alimupenda sana Daudi.


Yule kijana alipokwisha kuondoka, Daudi akasimama na kutoka pahali alipojificha karibu na lundo la mawe. Aliinama chini kwa heshima mara tatu mbele ya Yonatani. Wote wawili, Daudi na Yonatani, wakakumbatiana na kulia. Daudi alikuwa na uchungu zaidi kuliko Yonatani.


Halafu Yonatani akamwambia Daudi: “Uende na amani. Tumekwisha wote kuapa kwa jina la Yawe kwamba Yawe akuwe mushuhuda kati yetu milele, na kati ya wazao wangu na wazao wako milele.”


Kwa nini ninyi wote mumenifanyia shauri baya? Hakuna hata mumoja wenu anayeniambia habari hii, wakati mwana wangu anapofanya mapatano na mutoto wa Yese. Tena, kwa nini hakuna hata mumoja kati yenu anayesikitika au kunielezea kwamba mwana wangu mwenyewe anamuchochea mutumishi wangu juu yangu akinivizia kama inavyokuwa leo hii?”


Hao wote wawili, wakafanya agano mbele ya Yawe. Daudi akabaki katika muji wa Horeshi na Yonatani akaenda zake kwenye nyumba.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ