Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 18:27 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

27 Daudi na watu wake walikwenda, wakawaua Wafilistini mia mbili na kuyatwaa magovi yao mpaka kwa mufalme Saulo. Hapo akamuhesabilia hesabu kamili kusudi mufalme akuwe baba mukwe wa Daudi. Hivyo, Saulo akamupatia Daudi binti yake Mikali akuwe muke wake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 18:27
8 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Daudi akamujibu: “Ni vizuri, nitafanya agano nawe. Lakini ninakuomba jambo moja kwamba mbele haujaniona sharti kwanza uniletee Mikali binti ya Saulo. Hapo utaniona.”


Daudi vilevile alituma wajumbe kwa Isiboseti mwana wa Saulo akisema: “Unirudishie muke wangu Mikali ambaye nilimwoa kwa magovi mia moja ya Wafilistini.”


Hapo roho wa Yawe akamushika Samusoni kwa nguvu, naye akaenda muji Askeloni, akawaua watu makumi tatu, kisha akatwaa nguo zao za sikukuu, akawapa wale waliotegua kitendawili chake. Halafu akaondoka, akaenda kwa nyumba kwa wazazi wake akiwa na hasira kali.


Wana wa Saulo walikuwa: Yonatani, Iswi na Malkisua. Wabinti zake walikuwa wawili; muzaliwa wa kwanza aliitwa Merabu na mudogo aliitwa Mikali.


Hivyo, Saulo akamwondoa na kumufanya kiongozi wa waaskari elfu moja. Naye Daudi akawaongoza vyema katika vita.


Saulo akamwambia Daudi: “Huyu ni Merabu, binti yangu mukubwa, nitamutoa kwako kusudi umwoe kwa masharti mawili: Ukuwe askari wangu shujaa na mutiifu, upigane vita ya Yawe.” Saulo alizani kwa njia hiyo Wafilistini watamwua Daudi, kusudi kitendo hicho asikifanye yeye mwenyewe.


Lakini Saulo alipoona wazi kwamba Yawe alikuwa pamoja na Daudi, na kwamba Mikali binti yake alimupenda sana Daudi,


Wakati huo, Saulo alikuwa amemwoesha binti yake Mikali, ambaye alikuwa muke wa Daudi, kwa Palti mwana wa Laisi, wa muji wa Galimu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ