Lakini mufalme aliwatwaa wana wawili ambao Risipa binti ya Ahiya alimuzalia Saulo, nao ni: Armoni na Mefiboseti. Aliwatwaa vilevile watoto wote watano wanaume wa Mikali binti ya Saulo ambao alimuzalia Adrieli mwana wa Barzilayi wa muji Mehola.
Naye Yehu mwana wa Nimusi, umupakae mafuta akuwe mufalme wa Israeli. Elisha mwana wa Safati wa Abeli-Mehola, utamupakaa mafuta akuwe nabii kwa pahali pako.
Watu wa Gideoni walipopiga baragumu zao mia tatu, Yawe akawafanya Wamidiani waanze kuuana wao kwa wao katika kambi. Waliobaki wakatoroka mpaka Zerera, wakafika Beti-Sita, hata kwenye mupaka wa Abeli-Mehola karibu na Tabati.