Zamani, Saulo alipokuwa mufalme wetu wewe ndiwe uliyewaongoza Waisraeli katika vita, na Yawe alikuambia: ‘Utakuwa muchungaji wa watu wangu Waisraeli; utakuwa mukubwa juu ya inchi ya Israeli.’ ”
Ee Yawe, Mungu wangu, umeniweka mimi mutumishi wako kuwa mufalme pahali pa baba yangu Daudi, ijapokuwa ningali mutoto mudogo na sijui namna ya kutimiza kazi hii.
Mordekayi, Muyuda, alikuwa wa kwanza chini ya mufalme Ahasuero katika madaraka. Alipendwa na kuheshimiwa na Wayuda, maana alitumika kwa faida na amani ya watu wake na wazao wao wote.
Kokote Daudi alikotumwa na Saulo, Daudi alifanikiwa. Hivyo, Saulo akamufanya kuwa mukubwa wa waaskari wake. Jambo hilo liliwafurahisha watu wote hata watumishi wa Saulo.