Yule mukubwa wa kifungo hakujishugulisha tena na kitu chochote Yosefu alichopewa kwa maana Yawe alikuwa pamoja na Yosefu na kufanikisha kila kitu alichofanya.
Halafu Daudi akaweka kambi za waaskari katika muji wa Damasiki wa Aramu. Basi Waaramu wakakuwa watumishi wake, na wakakuwa wanalipa kodi. Yawe akamupa Daudi ushindi kokote alikokwenda.
kwa maana mimi ni pamoja nawe. Hakuna mutu katika muji huu atakayesubutu kukukamata kwa kukutendea vibaya, kwa maana ndani yake kutakuwa watu wengi watakaonigeukia.”
Yawe alikuwa pamoja na watu wa kabila la Yuda, nao wakaiteka inchi ya milima. Lakini hawakuweza kuwashinda wenyeji wa inchi ya bonde kwa sababu magari yao ya vita yalikuwa ya chuma.
Kijana mumoja kati ya watumishi akasema: “Nimemwona kijana mumoja wa Yese, wa muji wa Betelehemu. Kijana yule ana ujuzi wa kupiga kinubi. Yule kijana ni shujaa, hodari wa kupigana katika vita, ana hekima katika kusema na mwenye umbo zuri; Yawe yuko pamoja naye.”
Kisha kulikuwa vita tena kati ya Wafilistini na Waisraeli. Daudi alitoka akapigana na Wafilistini, akawaua Wafilistini wengi na waliobaki wakamukimbia.