Saulo alipomwona Daudi akienda kupigana na yule Mufilistini Goliati, alimwuliza Abeneri, jemadari wa kundi lake: “Abeneri, huyu ni kijana wa nani?” Abeneri alijibu: “Ee Mufalme, ninaapa kwa jina lako, mimi sijui.”
Mara tu Daudi aliporudi katika kambi nyuma ya kumwua Goliati, Abeneri alimukamata na kumupeleka kwa Saulo. Wakati ule Daudi alikuwa angali akibeba kichwa cha Goliati katika mikono yake.
Basi, Daudi akamwambia Ahimeleki: “Una upanga au mukuki ambao unaweza kunipatia? Kwa maana shuguli za mufalme zilinilazimisha niondoke haraka, nami niliondoka bila upanga wangu wala silaha nyingine yoyote.”