1 Samweli 17:50 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
50 Ndivyo Daudi alivyomushinda Goliati kwa mujeledi wake na jiwe. Alimupiga yule Mufilistini na kumwua. Daudi hakukuwa na upanga wowote katika mukono wake.
Nyuma ya Ehudu mwana wa Anati, Samugari akakamata nafasi yake. Yeye aliwaua Wafilistini mia sita kwa fimbo ya kuchunga ngombe. Naye vilevile aliwakomboa Waisraeli.
Kwa hiyo, siku ya vita hakuna mutu kati ya wote waliokuwa pamoja na Saulo na Yonatani aliyekuwa na upanga au mukuki isipokuwa Saulo na mwana wake Yonatani.
Daudi akajifunga upanga wa Saulo, akajaribu kutembea; lakini akashindwa kwa sababu hakuzoea nguo kama hizo. Akamwambia Saulo: “Siwezi kwenda katika vita nikiwa nimevaa nguo hizi, maana mimi sijazizoea.” Kwa hiyo, akazivua.
Akatia mukono wake ndani ya mufuko wake, akatoa jiwe moja, akalirusha kwa mujeledi wake, akamupiga nalo Goliati kwenye paji la uso wake, jiwe likalipasua paji la Goliati na kupenya ndani. Goliati akaanguka uso mpaka chini.
Basi, akaenda mbio, akasimama juu ya Goliati, akachomoa upanga wa Goliati toka katika mufuko wake, akamwua Goliati kwa kumukata kichwa chake. Wafilistini walipoona kwamba shujaa wao ameuawa, wakakimbia mbio.
Alipomwua yule Mufilistini Goliati, alihatarisha maisha yake, naye Yawe aliwapa Waisraeli ushindi mukubwa. Wewe ulipoona jambo lile ulifurahi. Kwa nini unataka kutenda zambi kwa kumwanga damu isiyokuwa na kosa kwa kumwua Daudi bila sababu?”
Basi, Daudi akamwambia Ahimeleki: “Una upanga au mukuki ambao unaweza kunipatia? Kwa maana shuguli za mufalme zilinilazimisha niondoke haraka, nami niliondoka bila upanga wangu wala silaha nyingine yoyote.”