Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 17:46 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

46 Siku ya leo, Yawe atakutia katika mikono yangu. Nitakushinda, nitakukata kichwa chako; na miili ya waaskari wa Wafilistini nitawapa ndege na nyama wa pori. Halafu dunia nzima itajua kwamba Mungu yuko katika Israeli.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 17:46
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nyuma ya siku tatu mufalme atakunyanyua kutoka katika kifungo, atainua kichwa chako kusudi akutundike juu ya muti, nao ndege watakula mwili wako.”


Halafu Ahimasi akamwambia mufalme kwa sauti kubwa: “Mambo yote ni sawa.” Akainama mbele ya mufalme, kwa heshima na kusema: “Yawe atukuzwe, Mungu wako, ambaye amekukomboa kutoka watu walioinua mikono yao juu yako, bwana wangu mufalme.”


Kisha, Risipa binti ya Aya alitwaa nguo ya gunia, akajitandikia juu ya jiwe kubwa. Alikaa pale tangu mwanzo wa mavuno mpaka wakati wa mvua ulipofika na kuinyeshea maiti. Wakati huo wote, aliwafukuza ndege na wanyama wa pori, usiku na muchana, kusudi wasifikie maiti hizo.


usikilize kutokea kwako mbinguni. Umujalie yule mugeni yote atakayokulilia, kusudi watu wote katika ulimwengu wapate kujua jina lako na kukutii kama watu wako Waisraeli wanavyofanya, na wapate kufahamu kwamba nyumba hii ambayo nimeijenga, inajulikana kwa jina lako.


Nayo mataifa yote katika ulimwengu yatajua kwamba kweli Yawe ndiye Mungu wala hakuna mwingine.


Sasa, ee Yawe, Mungu wetu, utuokoe toka katika makucha ya Saniharibu, kusudi falme zote za dunia zijue kwamba ni wewe tu, ee Yawe peke yako, ee Yawe, ambaye ni Mungu.”


Halafu akarudi kwa mutu wa Mungu pamoja na watu wake, akasema: “Sasa ninajua kwamba hakuna Mungu yeyote katika dunia lakini tu Mungu wa Israeli; kwa hiyo, tafazali sasa upokee zawadi ya mutumishi wako.”


Nitashangilia na kufurahia wema wako, maana wewe unaona taabu yangu, unajua huzuni yangu.


Anakomesha vita popote katika dunia. Anavunjavunja pinde na mikuki, nayo magari ya vita anayateketeza.


Lakini nimewaacha muishi kwa kuonyesha uwezo wangu. Kwa hiyo dunia yote itatambua kwamba mimi ni nani.


Sasa, ee Yawe, Mungu wetu, utuokoe toka katika makucha ya Saniharibu, kusudi falme zote za dunia zijue kwamba ni wewe peke yako, ee Yawe, ambaye ni Mungu.”


Yawe ameonyesha nguvu yake tukufu, mbele ya mataifa yote. Atawaokoa watu wake, na ulimwengu wote utashuhudia.


Enyi nyama wote wakali, nanyi nyama wote wa pori, mukuje mukule.


Vilevile kwa nafasi hii nitaivuruga mipango ya watu wa Yuda na ya watu wa Yerusalema. Nitawatoa washindwe na kuuawa kwa panga na waadui zao, wale wanaovizia maisha yao. Nazo maiti zao nitaziacha kuwa chakula cha ndege na nyama wa pori.


Watatiwa katika mikono ya waadui zao, na katika mikono ya watu wanaotaka kuwaua. Maiti zao zitakuliwa na ndege na nyama wa pori.


Mufalme akamwambia Danieli: Hakika, Mungu wako ni Mungu wa miungu na Bwana wa wafalme, na ndiye anayefumbua mafumbo kwa sababu ameweza kunifumbulia fumbo hili.


Kwa hiyo, ninaamuru kwamba watu wa kabila lolote, taifa lolote au luga yoyote, watakaosema kitu chochote cha kumuzarau Mungu wa Sadiraki, Mesaki na Abedenego, watakatwa vipandevipande na nyumba zao zitabomolewa. Maana hakuna mungu mwingine anayeweza kuokoa namna hii.


“Nafasi yoyote kunapokuwa muzoga, ndipo tai wanapokusanyika.


Maiti zenu zitakuwa chakula cha ndege wala hakutakuwa mutu atakayewafukuza.


Vilevile, kisha Yawe, Mungu wenu, kuyatia katika mikono yenu, mutayashinda na kuyaangamiza kabisa. Musifanye agano lolote nayo wala musiyahurumie.


Yawe, Mungu wenu, atawatia waadui zenu katika mikono yenu na atawafanya wahangaike mpaka waangamie.


Yawe akamwambia Yoshua: “Usiwaogope hata kidogo maana nimewatia katika mikono yako, wala hakuna hata mumoja atakayeweza kukushinda.”


kusudi watu wote wa dunia wajue kwamba mukono wa Yawe una nguvu; nanyi mupate kumwogopa Yawe, Mungu wenu, milele.”


Yonatani akamwambia yule kijana aliyemubebea silaha: “Kuja, tuende kwenye ile kambi ya hawa watu wasiotahiriwa. Labda Yawe atatusaidia, maana Yawe haokoi kwa kutegemea wingi au uchache wa watu.”


Mufilistini akamwambia Daudi: “Kuja kwangu! Mwili wako nitawapa ndege na nyama wa pori!”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ