42 Yule Mifilistini alipoangalia na kumwona vizuri Daudi, alimuzarau, maana Daudi alikuwa kijana muzuri mwenye afya nzuri na wa kupendeza.
Beni-Hadadi akawaambia: “Muwakamate wakiwa wazima. Hata kama wanakuja kwa vita au kwa amani.”
Kiburi kinatangulia maangamizi; majivuno yanatangulia maanguko.
Hivyo, Yese alituma mutu, naye akaletwa. Yule kijana alikuwa mwenye afya, mwenye macho yenye kungaa na wa kupendeza. Yawe akamwambia Samweli: “Sasa, huyu ndiye; simama umupakae mafuta.”
Saulo akamwambia Daudi: “Wewe hauwezi kwenda kupigana na Mufilistini yule. Wewe ni kijana tu, lakini mutu yule amekuwa katika vita tangu ujana wake.”
Yule Mufilistini, naye akaanza kumwendea Daudi, na yule aliyemubebea ngao yake akiwa mbele yake.