Vilevile, akamwua Mumisri mumoja, urefu wake ulikuwa metre mbili na nusu, naye alikuwa akibeba mukuki mukubwa sana katika mukono wake, kama muti wa mufumaji wa nguo. Lakini Benaya akamushambulia akiwa na fimbo tu, akamunyanganya mukuki ule, na kumwua Mumisri yule kwa mukuki wake mwenyewe.
Hata hivyo, enyi watu wangu, kwa ajili yenu, niliwaangamiza kabisa Waamori ambao walikuwa wakubwa kama mierezi, wenye nguvu kama miti ya mialo. Niliwaangamiza, matawi na mizizi.
(Mufalme Ogi ndiye peke yake aliyebakia kati ya Warefai. Kitanda chake kilichotengenezwa kwa chuma, kilikuwa na urefu wa metre ine na upana wa karibu metre mbili. Kitanda hicho kipo katika muji wa Waamori wa Raba.)
Alipokuwa anaongea nao, Goliati, yule shujaa wa Wafilistini kutoka Gati, alijitokeza mbele ya waaskari wa Israeli kama vile alivyozoea. Naye Daudi alimusikiliza vizuri sana.