Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 17:37 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

37 Yawe ambaye ameniokoa toka katika makucha ya simba na dubu, ataniokoa kutoka kwa Mufilistini huyu.” Saulo akamwambia: “Kwenda, naye Yawe akuwe pamoja nawe.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 17:37
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini ujipe moyo! Tupigane kama wanaume kwa ajili ya watu wetu na kwa ajili ya miji ya Mungu wetu. Naye Yawe atutendee lile analoona ni jema kwake.”


“Sasa, mwana wangu, Yawe, Mungu wako, akuwe pamoja nawe kusudi uweze kumujengea nyumba kama vile alivyosema.


wa kufua zahabu, feza, shaba na chuma. Basi sasa, anza kazi! Yawe akuwe pamoja nawe!”


Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi. Yawe ni kimbilio langu; namna gani basi munaweza kuniambia: “Ruka kama ndege, mpaka kwenye milima,


Yawe yuko nami, siogopi kitu; mwanadamu ataweza kunifanya nini?


Nilipokulilia, wewe ulinijibu; umeniongezea nguvu yangu.


Ninakukumbuka ninapokuwa katika kitanda, ninafikiri juu yako usiku kucha,


Kisha nikasema: “Kinachoniumiza zaidi ni kwamba Mungu Mukubwa hatendi tena kitu kwa ajili yetu!”


Mungu wetu ambaye tunamutumikia anaweza kutuokoa. Atatuokoa kutoka furu la moto mukali na vilevile kutoka katika mikono yako, ee mufalme.


Kama vile tulivyomutii Musa katika mambo yote, ndivyo tutakavyokutii wewe; Yawe, Mungu wako, akuwe pamoja nawe kama alivyokuwa pamoja na Musa.


Nyuma ya muda, Boazi akafika kutoka Betelehemu, akawasalimia wavunaji, akasema: “Yawe akuwe nanyi.” Nao wakamujibu: “Yawe akubariki.”


Mimi mutumishi wako nimekwisha kuua simba wengi na dubu wengi. Sasa, hata yule Mufilistini mupagani, ambaye amewatukana waaskari wa Mungu Mwenye Uzima, atakuwa kama wao.


Saulo akamuvalisha Daudi nguo zake za kivita, akamuvalisha kofia yake ya shaba juu ya kichwa na koti lake la kifua.


Yawe aniue ikiwa Saulo anakusudia kukuzuru nami nisipokujulisha kusudi uende pahali pa mbali ambapo utakuwa salama. Yawe akuwe pamoja nawe kama alivyokuwa pamoja na baba yangu.


Leo, umeonyesha jinsi unavyokuwa muzuri kwangu. Haukuniua ijapokuwa Yawe alinitia katika mikono yako.


Saulo akamwambia Daudi: “Mungu akubariki mwana wangu Daudi. Utafanya mambo makubwa, nawe utafanikiwa katika yote.” Basi, Daudi akaenda zake; Saulo naye akarudi kwake.


Kisha, Samweli alitwaa jiwe na kulisimamisha kati ya Misipa na Seni, akaliita jiwe hilo “jiwe la musaada”, akisema: “Yawe ametusaidia mpaka sasa.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ