Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 17:28 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

28 Lakini Eliabu, kaka mukubwa wa Daudi alipomusikia Daudi akiongea na watu, alimukasirikia Daudi, akasema: “Kwa nini umekuja? Wale kondoo wachache umemwachia nani kule katika mbuga? Ninajua majivuno yako na uovu wa moyo wako. Umekuja tu kutazama vita.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 17:28
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wandugu zake wakamwonea wivu, lakini baba yake akakuwa anafikiri juu ya jambo hilo.


Lakini wandugu zake walipoona kwamba baba yao alimupenda Yosefu kuliko wao, wakamuchukia hata hawakuzungumuza naye kwa amani.


Wandugu zake wakamwuliza: “Unataka kutuambia kwamba utatutawala? Au utakuwa na mamlaka juu yetu?” Basi, wakazidi kumuchukia kwa sababu ya ndoto na maneno yake.


Rehoboamu alioa muke, jina lake Mahalati binti ya Yeremoti mwana wa Daudi. Mama yake aliitwa Abihaili binti ya Eliabu, mwana wa Yese.


Washuhuda wakorofi wanajitokeza, wananiuliza mambo nisiyoyajua.


Ndugu aliyetendewa kosa ni mugumu kuliko muji wenye ukuta; magomvi yanakaza kama vile vifungio vya mulango wa ukuta.


Kasirani ni kali na hasira inaangamiza; lakini ni nani anayeweza kupingana na wivu?


Tena nilitambua kwamba mutu anatoa jasho na kutumia ujuzi wake juu ya wivu tu kwa mwenzake. Hayo nayo ni bure sawa na kutaka kukamata upepo.


na adui wa mutu atakuwa wa jamaa yake mwenyewe.


Alisema vile kwa maana alijua kwamba walimutoa Yesu kwake kwa sababu walimwonea wivu tu.


Wandugu zake za jamaa waliposikia maneno haya, wakaondoka kwenda kumutwaa, kwa maana walisema kwamba amepotelewa na akili.


Lakini watu hawa wanasema vibaya juu ya mambo wasiyoyafahamu; na mambo wanayoyajua kwa tabia yao kama nyama wasiokuwa na akili, ndiyo yale yanayowaangamiza.


Samweli akatwaa pembe lake lenye mafuta akamupakaa Daudi mafuta mbele ya kaka zake. Mara moja roho wa Yawe akamushika Daudi kwa nguvu na kuwa naye tangu siku hiyo. Kisha Samweli akarudi katika muji wa Rama.


Lakini Yawe alimwambia: “Usiangalie sura yake wala urefu wake. Mimi nimemukataa maana siangalii mambo kama vile wanadamu wenye kufa wanavyoangalia. Mwanadamu anaangalia umbo la inje, lakini mimi ninaangalia ndani ya moyo.”


Daudi akamujibu: “Sasa nimefanya nini? Siwezi kuuliza neno tu?”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ