Watu wenu elfu moja watamukimbia askari mumoja adui; na waaskari watano waadui watawakimbiza ninyi wote. Kwa mwisho, watakaobaki, watakuwa kama muti wa bendera kwa mulima, kama kitambulisho kinachokuwa juu ya kilima.
Mufalme wa Yuda alipopata habari kwamba Waaramu wanashirikiana na Waisraeli, yeye pamoja na watu wote wa Yuda waliogopa na kutetemeka kama miti inayotikiswa na upepo.
Na kwa njia ya wamoja wenu watakaobaki nitaleta woga ndani ya moyo wao, katika inchi ya waadui zao hata jani linalopeperushwa litawakimbiza. Watakimbia kama mutu anayekimbia vita. Watakimbia na kuanguka hata kama hakuna mutu anayewafukuza.
Mutu mumoja anaweza namna gani kuwashinda watu elfu moja, au watu wawili wanaweza namna gani kuwashinda watu elfu kumi, isipokuwa kama mulinzi wao amewatupa, Yawe amewaacha?
Alipokuwa anaongea nao, Goliati, yule shujaa wa Wafilistini kutoka Gati, alijitokeza mbele ya waaskari wa Israeli kama vile alivyozoea. Naye Daudi alimusikiliza vizuri sana.
Waliambiana: “Mumemwona yule mutu aliyejitokeza? Yeye amejitokeza kwa kuwazarau Waisraeli. Mufalme Saulo atamupa mutu yeyote atakayemwua mutu yule utajiri mwingi. Zaidi ya yote, atamupatia vilevile binti yake kusudi amwoe. Tena, watu wa jamaa ya baba yake watakuwa huru, hawatalipa kodi.”