Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 17:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Kesho yake, Daudi aliamuka asubui mapema, na akamwachia muchungaji mumoja kondoo. Alibeba chakula na kwenda kama vile alivyoagizwa na baba yake Yese. Alipofika kwenye kambi ya Waisraeli, aliwakuta wanajipanga kwenye sehemu yao ya vita na wanapiga kelele za vita.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 17:20
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa maana siku zitakufikia wakati waadui zako watakapokuzunguka kwa vita, watakapojenga ukuta wa kujikingia pembeni yako, na kukusonga pande zote.


Asubui mapema Yoshua pamoja na watu wote wa Israeli walianza safari kutoka Sitimu. Walipofika kwa muto Yordani, walipiga kambi hapo kwa muda mbele ya kuvuka.


Samweli alisikia kwamba Saulo alikuwa amekwenda kule Karmeli na amesimamisha munara wa ukumbusho wake, na kwamba amekwenda Gilgali. Hivyo, kesho yake, Samweli aliamuka asubui mapema, akaenda kukutana na Saulo.


Wakati ule, mufalme Saulo, kaka za Daudi na waaskari wote wa Israeli walikuwa kwenye bonde la Ela, wanapigana na Wafilistini.


Makundi ya waaskari ya Waisraeli na ya Wafilistini walijipanga tayari kupigana vita, makundi yakiwa yanaangaliana uso kwa uso.


Lakini Eliabu, kaka mukubwa wa Daudi alipomusikia Daudi akiongea na watu, alimukasirikia Daudi, akasema: “Kwa nini umekuja? Wale kondoo wachache umemwachia nani kule katika mbuga? Ninajua majivuno yako na uovu wa moyo wako. Umekuja tu kutazama vita.”


Daudi akatoka, akaenda pahali Saulo alipopiga kambi. Akaona pahali ambapo Saulo alikuwa amelala. Saulo alikuwa pamoja na Abeneri mwana wa Neri, mukubwa wa waaskari, katikati ya kambi akizungukwa na waaskari wake.


Kwa hiyo usiku, Daudi na Abisai wakaingia kwenye kambi ya Saulo, wakamukuta Saulo amelala katikati ya kambi hiyo, na mukuki wake umechomekwa katika udongo karibu na kichwa chake. Abeneri pamoja na waaskari walikuwa wamelala na kumuzunguka Saulo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ