Ahimeleki akamujibu: “Upanga wa Goliati Mufilistini uliyemwua kwenye bonde la Ela uko nyuma ya efodi, unafungwa katika kitambaa. Ikiwa unataka kuukamata basi, uukamate maana hakuna upanga mwingine hapa.” Daudi akamwambia: “Hakuna upanga mwingine kama huo; unipe.”
Basi, Daudi akamwambia Ahimeleki: “Una upanga au mukuki ambao unaweza kunipatia? Kwa maana shuguli za mufalme zilinilazimisha niondoke haraka, nami niliondoka bila upanga wangu wala silaha nyingine yoyote.”