1 Samweli 17:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
17 Siku moja, Yese alimwambia mwana wake Daudi: “Uwapelekee kaka zako kilo kumi za ngano yenye kukaangwa na mikate kumi. Uwapelekee haraka kule katika kambi.
Basi ikiwa ninyi munaokuwa waovu munajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, zaidi sana Baba yenu anayekuwa mbinguni atawapa wale wanaomwomba vitu vizuri zaidi.
Basi ikiwa ninyi munaokuwa waovu munajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, inaonyesha hakika kwamba Baba yenu anayekuwa mbinguni atawapa Roho Mutakatifu wale wanaomwomba kwake.”
Wakati wa chakula, Boazi akamukaribisha Ruta akamwambia: “Karibu hapa, kuja ukule mukate vilevile na uuchovye ndani ya divai.” Kwa hiyo Ruta akaikaa pamoja na wavunaji, na Boazi akamupa ngano iliyokaangwa, akakula akashiba hata akaacha sehemu.
Abigaili akafanya haraka, akatwaa mikate mia mbili, mifuko miwili ya ngozi ya mbuzi yenye kujaa divai, kondoo watano waliotayarishwa vizuri, kilo kumi na saba za ngano zenye kukaangwa, vishada mia moja vya zabibu zenye kukauka, mikate ya tini mia mbili, na vitu hivi vyote akavipakia juu ya punda.