Mulimwogopa na kutishwa na nani hata mukasema uongo, mukaacha kunikumbuka mimi na kuacha kabisa kufikiri juu yangu? Mimi sikuwaambia kitu kwa muda murefu; ndiyo maana labda mukaacha kuniheshimu!
Kumbuka kwamba mimi nimekuamuru ukuwe imara na hodari. Usiogope wala usifazaike kwa sababu mimi Yawe, Mungu wako, niko pamoja nawe popote utakapoenda.”
Wengine walivuka muto Yordani mpaka katika inchi ya Gadi na inchi ya Gileadi. Lakini Saulo alikuwa angali kule Gilgali pamoja na watu wote waliomufuata wakitetemeka.
Daudi alikuwa mutoto wa Yese, wa ukoo wa Efurata kutoka Betelehemu katika inchi ya Yuda. Yese alikuwa na watoto wanane wa kiume. Wakati Saulo alipokuwa mufalme, yeye alikuwa amekwisha kuwa muzee, mutu mwenye umri mukubwa.