Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 16:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Lakini Yawe alimwambia: “Usiangalie sura yake wala urefu wake. Mimi nimemukataa maana siangalii mambo kama vile wanadamu wenye kufa wanavyoangalia. Mwanadamu anaangalia umbo la inje, lakini mimi ninaangalia ndani ya moyo.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 16:7
34 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

lakini hakupendezwa na Kaina wala na sadaka yake. Basi, Kaina akakasirika sana na uso wake ukakunjamana.


Katika inchi yote ya Israeli, hakuna mutu yeyote aliyesifiwa kwa uzuri wa umbo kama Abusaloma. Tangia kwenye miguu mpaka kwenye kichwa, Abusaloma hakukuwa na kilema chochote.


Nikuambie nini zaidi, mimi Daudi? Maana wewe unanijua mimi mutumishi wako, ee Bwana wangu Yawe!


basi, usikilize kule kwako mbinguni, uwasamehe na kumutendea kila mutu kwa kadiri anavyostahili, maana ni wewe tu unayejua mawazo ya mioyo ya wanadamu wote,


Nikuambie nini zaidi, mimi Daudi mutumishi wako, kwa kunitukuza vile? Wewe unanijua mimi mutumishi wako.


“Nawe Solomono mwana wangu, umujue Mungu wa baba yako, na umutumikie kwa moyo wako wote na kwa nia nzuri; yeye Yawe anachunguza mioyo na anafahamu mipango na mafikiri ya mwanadamu. Ukimutafuta yeye, utamwona; lakini ukimwacha, atakutupilia mbali milele.


Yawe anachunga kwa uangalifu ulimwengu wote, kwa kuwapa nguvu wale wanaokuwa waaminifu kwake. Umetenda jambo la kipumbafu, kwa hiyo tangu sasa, utakuwa na vita kila mara.”


basi usikilize kutokea kule mbinguni, utoe musamaha, vilevile umutendee kila mutu kadiri anavyostahili, (maana ni wewe tu unayejua mawazo ya mioyo ya wanadamu wote),


Uko na macho kama ya mwanadamu? Unaona kama vile mwanadamu anavyoona?


Basi uangalie mbingu! Angalia mawingu yanayokuwa juu kuliko wewe!


Nikiikaa au nikisimama, wewe unajua; wewe unajua kila kitu ninachofikiri juu yake.


Wewe, ee Yawe, unayehukumu mataifa, unihukumu kadiri ya haki yangu, kulingana na ukamilifu wangu.


Ikiwa Yawe anajua kuzimu na shimo la kuangamia, mawazo ya mwanadamu yataweza namna gani kujificha mbele yake?


Matendo yote ya mutu yanaonekana kwake kuwa sawa lakini Yawe anapima nia ya mutu.


Usiseme kisha: “Hatukujua!” Maana Mungu anayepima mioyo ya watu anaona; yeye atakulipa kulingana na matendo yako!


Mapendezi ni udanganyifu na uzuri wa uso haukawii, lakini mwanamuke anayemwogopa Yawe atasifiwa.


Lakini, ee Yawe wa majeshi, wewe unayehukumu kwa haki, unayechunguza mioyo na akili za watu, unijalie nione jinsi utakavyowalipiza kisasi, maana ninayaweka maneno yangu kwako.


Mimi Yawe ninapima akili na kuchunguza moyo wa mutu. Na hivyo ninamutendea kila mumoja, kulingana na mwenendo wake, kadiri ya matendo yake.


Ee Yawe wa majeshi, wewe unayemupima mutu wa haki, unayechunguza mioyo na akili ya watu, nione kisasi chako juu yao maana ninakutegemea kwa kunitetea.


Yesu akawaambia: “Ninyi ni watu wanaojionyesha kuwa wenye haki mbele ya watu, lakini Mungu anajua yanayokuwa ndani ya mioyo yenu. Kwa maana mambo yanayosifiwa na watu ni machukizo mbele ya Mungu.


Muache kuhukumu kufuatana na hali ya inje, lakini muhukumu kwa haki.”


Ninyi munahukumu kwa kufuatana na mafikiri ya kimutu; lakini mimi simuhukumu mutu.


Kisha wakaomba wakisema: “Bwana, wewe unayejua yanayokuwa ndani ya mioyo ya watu wote, utuonyeshe ni nani uliyemuchagua kati ya hawa wawili


Kwa sababu wengi wanasema: “Barua za Paulo ni kali na zenye maneno mazito; lakini yeye mwenyewe anapokuwa katikati yetu ni muzaifu na namna yake ya kusema ni ya kuzarauliwa.”


Ninyi munaangalia tu namna vitu vinavyoonekana kwa inje. Mutu yeyote anayejiaminia kwamba yeye ni wa Kristo, inafaa afikiri tena yeye mwenyewe mambo haya: ikiwa yeye ni wa Kristo sisi vilevile ni wa Kristo.


Hakuna kitu kinachoweza kufichwa mbele ya Mungu, lakini vitu vyote vinafunuliwa na viko wazi mbele ya macho yake, yeye tutakayemutolea hesabu ya maneno yetu.


Mumwendee Bwana. Yeye ni jiwe lenye uzima. Jiwe lile lilitupiliwa na watu lakini lilichaguliwa na Mungu, nalo linahesabiwa kuwa la bei kali mbele yake.


Lakini mapambo yenu yanapaswa kuwa ya ndani ya moyo yasiyoweza kuharibika. Sherti mapambo yale yakuwe yenye kutokana na roho ya amani na upole inayohesabiwa kuwa ya bei kali mbele ya Mungu.


Nitawaua wafuasi wake. Na hivi makanisa yote yatajua kwamba mimi ndiye ninayechunguza mioyo ya watu na mafikiri yao. Vilevile yatajua kwamba mimi nitamulipa kila mumoja wenu kufuatana na matendo yake.


Muache kujisifu, muache kusema kwa kiburi. Maana anayejua ni Yawe. Yeye anayapima matendo yote.


Kisi alikuwa na mwana aliyeitwa Saulo. Saulo alikuwa kijana mwenye sura nzuri, na hakuna mutu katika Israeli aliyelingana na Saulo kwa uzuri. Saulo alikuwa murefu zaidi kuliko mutu yeyote katika inchi ya Israeli; watu wote walimufikia kwenye mabega.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ