Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 16:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Samweli akawajibu: “Nimekuja kwa amani. Nimekuja kumutolea Yawe sadaka. Mujitakase wenyewe halafu tuende kutolea sadaka.” Samweli akamutakasa Yese pamoja na wana wake, akawakaribisha kwenye sadaka.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 16:5
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Yakobo akawaambia jamaa yake na wote aliokuwa nao: “Mutupilie mbali sanamu za miungu ya kigeni munazokuwa nazo, mujitakase na kubadilisha nguo zenu.


Nyuma, Adonia mwana wa Hagiti, alimwendea Batiseba, mama ya Solomono. Batiseba akamwuliza: “Unaleta habari ya amani?” Adonia akamujibu: “Ndiyo, ninaleta habari ya amani.


Daudi akatoka inje kwa kuwapokea, akawaambia: “Ikiwa mumekuja kwangu kama warafiki kwa kunisaidia basi ninawapokea kwa moyo wote, lakini kama mumekuja kwa kunitoa kwa waadui zangu, ingawa sijatenda ovu lolote, Mungu wa babu zetu awaone na kuwaazibu ninyi.”


Kila mara karamu ilipomalizika, Yobu aliita wana wake kusudi awatakase. Aliamuka asubui mapema kisha karamu, akatoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa ajili ya kila mumoja wao maana aliwaza: “Labda wana wangu wametenda zambi na kumutukana Mungu ndani ya mioyo yao.”


Yawe akamwambia Musa: “Kwenda kwa watu uwatakase leo na kesho. Uwaambie wafue nguo zao


Muwakusanye watu wote, muwatakase watu. Muwalete wazee, muwakusanye watoto, hata watoto wanaonyonya. Bwana-arusi na bibi-arusi watoke katika vyumba vyao.


Munyamaze mbele ya Bwana wenu Yawe, maana siku ya Yawe iko karibu. Yawe ametayarisha sadaka, naye amekwisha kutakasa waalikwa wake.


Watu walizungukazunguka na kuikusanya, kisha waliisaga kwa mawe ya kusagia au waliitwanga katika vinu, halafu waliitokotesha ndani ya vyungu na kutengeneza maandazi. Onjo yake ilikuwa kama ya maandazi yaliyokaangwa kwa mafuta.


Basi kila mutu ajichunguze mwenyewe na kisha akule mukate huu na kunywa kikombe hiki.


Yoshua akawaambia watu: “Mujitakase kwa sababu kesho Yawe atatenda maajabu kati yenu.”


Basi, simama uwatakase watu, uwaambie wajitakase na kujitayarisha kwa siku ya kesho, maana mimi Yawe, Mungu wa Israeli, ninasema hivi: ‘Kati yenu kuna vitu vilivyotolewa viangamizwe. Hamuwezi kuwashinda waadui zenu mpaka vitu hivyo vimeondolewa kati yenu!


Siku hiyo, Saulo hakusema neno lolote, maana alifikiri kwamba labda Daudi amepatwa na tatizo au yeye si safi kwa kuhuzuria sikukuu hiyo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ