Hapo Israeli, baba yao, akawaambia: “Basi! Kwa vile ni lazima ikuwe hivyo basi, mufanye hivi: mutwae katika mifuko yenu sehemu ya mazao bora ya inchi yetu, mumupelekee zawadi yule mukubwa. Mumupelekee mafuta kidogo ya mukwaju, asali kidogo, ubani, marasi, kungu na lozi.
Abigaili akafanya haraka, akatwaa mikate mia mbili, mifuko miwili ya ngozi ya mbuzi yenye kujaa divai, kondoo watano waliotayarishwa vizuri, kilo kumi na saba za ngano zenye kukaangwa, vishada mia moja vya zabibu zenye kukauka, mikate ya tini mia mbili, na vitu hivi vyote akavipakia juu ya punda.