Sasa, ee bwana wetu, amuru watumishi wako wanaokutumikia wamutafute mutu mwenye ufundi wa kupiga kinubi, na huyo pepo muchafu kutoka kwa Mungu atakapokufikia, mutu yule atapiga kinubi, nawe utapata utulivu.”
Kijana mumoja kati ya watumishi akasema: “Nimemwona kijana mumoja wa Yese, wa muji wa Betelehemu. Kijana yule ana ujuzi wa kupiga kinubi. Yule kijana ni shujaa, hodari wa kupigana katika vita, ana hekima katika kusema na mwenye umbo zuri; Yawe yuko pamoja naye.”