Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 16:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Kisha roho wa Yawe alimwacha Saulo, na pepo muchafu kutoka kwa Yawe akamusumbua.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 16:14
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini sitaacha kumutendea mema yangu kama vile nilivyoacha kwa Saulo, niliyemwondoa mbele yako.


Kisha Mikaya akasema: “Sasa sikia neno la Yawe: Nilimwona Yawe akiikaa katika kiti chake cha kifalme, na jeshi lote la mbinguni likisimama pembeni yake, upande wake wa kuume na wa kushoto.


Yawe akamwuliza: ‘Kwa namna gani?’ Naye akajibu: ‘Nitakwenda na kuwasukuma manabii wake wote waseme uongo.’ Yawe akamwambia: ‘Wewe utamushawishi na utashinda; basi, kwenda ufanye hivyo.’


Ugeuke, usiangalie zambi zangu; uyafute makosa yangu yote.


Hata kama wakilea watoto, sitamwacha hata mumoja wao muzima. Ole kwao, nitakapowaacha peke yao!


Delila akamwambia Samusoni: “Samusoni! Wafilistini wanakuja kukushambulia!” Samusoni akaamuka toka katika usingizi naye akifikiri kwamba atatoka na kujiokoa kama vile mbele. Kumbe hakujua kwamba Yawe alikuwa amemwacha.


Samusoni akazishika nguzo mbili za katikati ambazo zilitegemeza uzito wote wa nyumba ile, mukono mumoja nguzo hii na mukono mwingine nguzo ya pili.


Kisha Mungu akaleta roho ya uadui kati ya Abimeleki na watu wa Sekemu, nao wakamwasi.


Mara moja, Saulo aliposikia maneno hayo, roho wa Mungu akamufikia kwa nguvu, naye akawaka hasira kali.


Halafu watumishi wa Saulo wakamwambia: “Tunajua kwamba pepo muchafu kutoka kwa Mungu anakusumbua.


Sasa, ee bwana wetu, amuru watumishi wako wanaokutumikia wamutafute mutu mwenye ufundi wa kupiga kinubi, na huyo pepo muchafu kutoka kwa Mungu atakapokufikia, mutu yule atapiga kinubi, nawe utapata utulivu.”


Kila mara, yule roho mwovu kutoka kwa Mungu alipomufikia Saulo, Daudi alitwaa kinubi chake na kuanza kukipiga, na roho yule alimwacha Saulo, naye akajisikia vizuri na kupata utulivu.


Kesho yake, pepo muchafu kutoka kwa Mungu akamushambulia Saulo kwa rafla, akakuwa anapayukapayuka kama mwenda-wazimu katika nyumba yake. Daudi alikuwa anapiga kinubi kama alivyofanya siku zote. Saulo alikuwa na mukuki katika mukono wake.


Saulo alikuwa anamwogopa Daudi kwa sababu Yawe alikuwa pamoja naye, lakini Yawe alikuwa amemwacha Saulo.


Samweli akamwambia Saulo: “Kwa nini unanisumbua kwa kunipandisha?” Saulo akamujibu: “Mimi nina taabu kubwa! Wafilistini wananishambulia kwa vita, na Mungu ameniachilia. Hanijibu tena kwa njia ya manabii wala kwa ndoto. Ndiyo maana nimekuita unijulishe kitu cha kufanya.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ