Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 16:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Samweli akatwaa pembe lake lenye mafuta akamupakaa Daudi mafuta mbele ya kaka zake. Mara moja roho wa Yawe akamushika Daudi kwa nguvu na kuwa naye tangu siku hiyo. Kisha Samweli akarudi katika muji wa Rama.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 16:13
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Natani akamwambia Daudi: “Wewe ndiwe mutu yule! Sasa, Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Mimi nilikupakaa mafuta ukuwe mufalme juu ya Israeli. Nilikuokoa toka katika mikono ya Saulo.


Watu wa Yuda walimwendea Daudi kule Hebroni wakamupakaa mafuta akuwe mufalme wao. Daudi aliposikia kwamba watu wa Yabesi-Gileadi ndio waliomuzika Saulo,


Haya ni maneno ya mwisho ya Daudi. Ni ujumbe wa Daudi mwana wa Yese, ujumbe wa mutu ambaye Mungu alimufanya akuwe mukubwa, muchaguliwa wa Mungu wa Yakobo, mwimbaji muzuri wa zaburi wa Israeli:


Basi, wazee wote wa Waisraeli wakamwendea mufalme Daudi kule Hebroni. Naye akafanya agano nao mbele ya Yawe, halafu wakamupakaa Daudi mafuta akuwe mufalme wa Israeli.


Halafu wote wawili wakaingia ndani ya chumba cha ndani na kule nabii akamutia Yehu mafuta juu ya kichwa na kumwambia: “Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Ninakupakaa mafuta ukuwe mufalme juu ya watu wangu Israeli.


Basi, wazee wote wa Waisraeli wakamwendea mufalme kule Hebroni; naye Daudi akafanya agano nao mbele ya Yawe, halafu wakamupakaa Daudi mafuta akuwe mufalme wa Waisraeli kulingana na neno la Yawe lililotolewa kwa njia ya Samweli.


Zamani ulisema katika maono, ukawaambia watumishi wako waaminifu: “Nimemupa nguvu shujaa mumoja, nimemwinua huyo niliyemuchagua kati ya watu.


Nimemupata mutumishi wangu Daudi; nimemuchagua kwa kumupakaa mafuta yangu matakatifu.


Nitashuka kule na kuzungumuza nawe; nitatwaa sehemu ya roho niliyokupa, niwape watu hao. Nao watabeba muzigo wa kuwatunza watu hawa pamoja nawe, kusudi usibebe muzigo huo peke yako.


Yawe akamwambia Musa: Umutwae Yoshua mwana wa Nuni, mutu mwenye roho nzuri, kisha uweke mikono juu yake,


Aliyetumwa na Mungu anasema maneno ya Mungu, kwa sababu Mungu anamujaza Roho wake kwa uwingi.


Kisha kumwondosha Saulo, Mungu akasimika Daudi kuwa mufalme wao. Na yeye mwenyewe alimushuhudia akisema: ‘Nimejichagulia Daudi mwana wa Yese, kwa maana ni mutu mwenye kunipendeza. Huyu ndiye atakayefanya mambo yote ninayotaka.’


Unapenda haki na kuchukia uovu. Ni kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekusimika, akikupakaa mafuta, akikupatia heshima na kukuinua juu kuliko wenzako wote.”


Basi niseme nini tena? Maana wakati hauniruhusu kueleza habari juu ya Gideoni, Baraka, Samsoni, Yefuta, Daudi, Samweli na manabii.


Kisha roho wa Yawe akamujaza Yefuta, naye akaondoka na kupitia Gileadi na Manase, akarudi Misipa katika inchi ya Gileadi na kuendelea mpaka Amoni.


Roho wa Yawe akaanza kumusukuma akiwa kule Mahane-Dani, kati ya muji wa Zora na wa Estaoli.


Basi, roho wa Yawe akamushika Samusoni kwa nguvu, akamurarua simba huyo kama mutu anavyorarua mwana-mbuzi. Naye Samusoni hakuwaambia wazazi wake jambo lile.


Basi, roho wa Yawe akamujaza Otinieli, naye akakuwa mwamuzi wa Waisraeli. Otinieli alikwenda katika vita naye Yawe akamutia Kusani, Yule-Mwovu-Sana, ufalme wa Mesopotamia, katika mikono yake.


Kesho yake asubui, Elekana na jamaa yake waliamuka asubui mapema, na kisha kumwabudu Yawe, walirudi kwao Rama. Elekana akalala na muke wake Hana na Yawe akamukumbuka.


Halafu Samweli akatwaa chupa ndogo ya mafuta akamumiminia Saulo juu ya kichwa, akamubusu na kumwambia: “Yawe amekutia mafuta ukuwe mutawala juu ya watu wake.


Roho wa Yawe atakufikia kwa nguvu, nawe utaanza kutabiri pamoja nao na kugeuka kuwa mutu mwingine.


Mara moja, Saulo aliposikia maneno hayo, roho wa Mungu akamufikia kwa nguvu, naye akawaka hasira kali.


Kijana mumoja kati ya watumishi akasema: “Nimemwona kijana mumoja wa Yese, wa muji wa Betelehemu. Kijana yule ana ujuzi wa kupiga kinubi. Yule kijana ni shujaa, hodari wa kupigana katika vita, ana hekima katika kusema na mwenye umbo zuri; Yawe yuko pamoja naye.”


Saulo alikuwa anamwogopa Daudi kwa sababu Yawe alikuwa pamoja naye, lakini Yawe alikuwa amemwacha Saulo.


Kisha, nitajiinulia kuhani mwingine mwaminifu atakayefanya kulingana na yale yanayokuwa ndani ya moyo na akili yangu. Nitamujengea ukoo imara, naye atatumika siku zote mbele ya mufalme wangu muchaguliwa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ