Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 15:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Saulo akawaambia Wakeni: “Muende! Muondoke! Mutoke kati ya Waamaleki, kama sivyo, nitawaangamiza pamoja nao. Muondoke kwa sababu ninyi muliwatendea mema Waisraeli walipotoka Misri.” Basi, Wakeni wakaondoka kati ya Waamaleki.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 15:6
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

ni kusema inchi za Wakeni, Wakenizi, Wakadimoni,


Sizani kama utafanya hivyo, kuwaua watu wa haki pamoja na waovu, kutendea watu wa haki sawa na waovu. Hapana, haiwezekani! Mwamuzi wa dunia yote hataacha kutenda mambo yanayokuwa sawa!”


Watu wa jamaa hizi waliishi katika muji wa Yabesi: Watirati, Wasimeati na Wasukati. Wao ndio Wakeni waliotoka katika uzao wa Hamati, aliyekuwa babu ya waliokuwa wa ukoo wa Warekabu.


Sikiliza shauri langu kwako na Mungu akuwe pamoja nawe. Wewe utawasimamia watu mbele ya Mungu na kumuletea Mungu matatizo yao.


Achana na ujinga upate kuishi; fuata njia ya akili.”


Waisraeli wote wengine waliokuwa karibu waliposikia vilio vyao wakakimbia wakisema: Tukimbie, kusudi udongo usitumeze na sisi vilevile.


Petro akazidi kusema maneno mengine ya kuwaonya na kuwatia moyo, akisema: “Mujiokoe toka kati ya kizazi hiki kipotovu!”


Kwa sababu hiyo Bwana anasema: “Mutoke kati yao, mujitenge nao. Musiguse kitu chochote kinachohesabiwa kuwa kichafu, nami nitawapokea.


Bwana awajalie mema sana watu wa jamaa ya Onesiforo, kwa maana amekuja mara nyingi kunifariji, wala hakusikia haya kwa kuniona niko katika kifungo.


Nao wale wachuuzi wanauambia muji ule: “Mazao mbalimbali uliyotamani sana kupata, yametoweka kwako. Na vitu vyote vya bei kali na vizuri vyenye kungaa vimekupotea, wala hautaviona tena.”


Wazao wa Keni ambaye alikuwa baba mukwe wa Musa, walifuatana na watu wa kabila la Yuda kutokea Muji wa Miti ya Ngazi, ni kusema muji wa Yeriko, mpaka jangwa la Yuda karibu na Aradi, wakafanya makao yao kule pamoja na watu wa Yuda.


Wakati ule, Mukeni mumoja aliyeitwa Heberi alikuwa amejitenga na Wakeni wenzake ambao ni wazao wa Hobabu, baba mukwe wa Musa. Alikuwa amepiga hema lake mbali kule kwenye muti wa mwalo wa Sananimu, karibu na Kedesi.


“Abarikiwe kuliko wanawake wote Yaeli, muke wa Heberi Mukeni. Amebarikiwa kuliko wanawake wote wanaokaa katika mahema.


Halafu yeye na watu wake wakaenda kwenye muji wa Amaleki, wakajificha wakivizia katika bonde.


Akisi alipomwuliza: “Leo mashambulizi yako yalikuwa juu ya nani?” Daudi alimwambia: “Juu ya Negebu ya Yuda” au “Juu ya Negebu ya Wayerameli” au “Juu ya Negebu ya Wakeni”.


wakaaji wa Rakali, wakaaji wa miji ya Wayerameli, wakaaji wa miji ya Wakeni,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ