Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 15:35 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

35 Tangu siku ile, Samweli hakumwona tena Saulo, mpaka siku alipokufa. Hata hivyo Samweli alimulilia Saulo. Naye Yawe alisikitika kwamba alikuwa amemusimika Saulo kuwa mufalme juu ya inchi ya Israeli.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 15:35
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe akasikitika sana kwa kumwumba mwanadamu katika dunia. Yawe akahuzunika sana ndani ya moyo wake.


Basi Mikali binti ya Saulo hakukuwa na mutoto mpaka kufa kwake.


Macho yangu yanatiririka machozi kama muto, kwa sababu watu hawaishiki sheria yako.


Ninapowaona waasi hao ninachukizwa sana, kwa sababu hawashiki amri zako.


Mimi nimewaambia mara nyingi, nami ninawaambia tena kwa machozi: kuna watu wengi wanaoonyesha kwa njia ya mwenendo wao kwamba kufa kwa Kristo juu ya musalaba ni chukizo kwao.


“Ninajuta kwamba nimemufanya Saulo kuwa mufalme. Yeye ameacha kunifuata mimi na hajatimiza amri zangu.” Samweli alikasirika, akamulilia Yawe usiku kucha.


Yawe akamwambia Samweli: “Utamulilia Saulo mpaka wakati gani? Wewe unajua kwamba mimi nimemukataa kuwa mufalme wa Israeli. Sasa, jaza ile pembe yako ya kuwekea mafuta, uondoke. Nitakutuma kwa Yese wa muji wa Betelehemu. Maana nimejipatia mufalme kati ya wana wake.”


Alivua nguo zake, akatabiri mbele ya Samweli. Alibaki uchi kwa siku moja, muchana na usiku. Kwa hiyo watu walianza kujiuliza: “Hata Saulo ni mumoja wa manabii?”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ