25 Lakini sasa ninakuomba, unisamehe zambi yangu. Uniruhusu nirudi pamoja nawe kusudi niweze kumwabudu Yawe.”
Kisha, Daudi akasimama, akaoga, akajipakaa mafuta na kubadilisha nguo zake. Halafu akaenda katika nyumba ya Yawe na kuabudu. Kisha akarudi kwake, akaamuru wamuletee chakula, naye akakula.
Kwa hiyo sasa ninawasihi munisamehe zambi yangu mara hii, muniombee kwa Yawe, Mungu wenu, aniondolee kifo hiki.”
Samweli akamujibu: “Siwezi hata kidogo kurudi pamoja nawe. Wewe umeikataa amri ya Yawe, naye amekukataa kuwa mufalme juu ya Israeli.”