Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 15:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

24 Saulo akamwambia Samweli: “Nimetenda zambi. Nimeasi amri ya Yawe na amri yako, kwa sababu niliwaogopa watu, nikawatii wao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 15:24
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yule mwanaume akajibu: “Mwanamuke uliyenipa akae pamoja nami ndiye aliyenipa tunda la muti ule, nami nikakula.”


Kisha akamwambia yule mwanaume: “Wewe umemusikiliza muke wako na kula matunda ya muti ambayo nilikuamuru usikule. Basi, udongo umelaaniwa kwa sababu yako. Kwa jasho utajipatia toka humo chakula chako, siku zote za maisha yako.


Basi, Daudi akamwambia Natani: “Nimetenda zambi mbele ya Yawe.” Natani akamwambia: “Yawe amekusamehe zambi yako, nawe hautakufa.


Sijaogopa kusimama mbele ya kundi la watu wala kukaa kimya au kujifungia ndani, kwa kuogopa kutishwa na mazarau yao.


Unisafishe kabisa kosa langu; unitakase zambi yangu.


Hapo mufalme wa Misri akaita Musa na Haruni kwa haraka, akawaambia: “Nimetenda zambi mbele ya Yawe, Mungu wenu, na mbele yenu.


Usifuate watu wengi kwa kutenda ubaya. Wala wakati wa kukata maneno, usishuhudie kufuatana na watu wengi kwa kupotosha haki.


Basi, mufalme wa Misri akaagiza Musa na Haruni waitwe, akawaambia: “Mara hii nimetenda zambi. Yawe ana haki na mimi na watu wangu tumekosa.


Kuogopa watu ni kujitega mwenyewe, lakini anayemutumainia Yawe yuko salama.


Mufalme Zedekia akasema: Basi! Mutu huyu yuko katika mikono yenu; mimi siwezi kuwapinga.


Balamu akamwambia malaika wa Yawe: Nimetenda zambi maana sikujua kwamba umesimama katika njia kwa kunizuia. Sasa, kama haikupendezi niendelee na safari hii, basi nitarudi kwangu.


Akawaambia: “Nimekosa kwa kumutoa mutu huyu asiyekuwa na kosa auawe.” Lakini wao wakamujibu: “Jambo hilo halituelekei. Ni kazi yako wewe mwenyewe!”


Basi kusema vile inaonyesha kwamba ninatafuta watu wanikubali? Hapana! Ninataka kukubaliwa na Mungu. Au ninatafuta kuwapendeza watu? Kama ningekuwa ningali ninatafuta kuwapendeza watu, singekuwa mutumishi wa Kristo.


Lakini watu wenye woga, wasioamini, wenye machukizo, wauaji, wazinzi, wachawi, wanaoabudu sanamu na wote wanaosema uongo, fungu lao ni katika lile ziwa la moto na ndani ya mawe ya kiberiti yanayowaka moto. Hiki ndicho kifo cha pili.”


Saulo akajibu: “Watu waliwaacha wazima kondoo na ngombe bora kabisa kwa kumutolea Yawe, Mungu wako, lakini wengine wote tumewaangamiza.”


Saulo akajibu: “Nimefanya zambi. Hata hivyo, uniheshimishe sasa mbele ya wazee wa watu wangu na Waisraeli. Uniruhusu nirudi pamoja nawe kusudi nimwabudu Yawe, Mungu wako.”


Lakini Saulo na watu wake hawakumwua Agagi, kondoo bora kabisa, ngombe wazuri, wana-ngombe, wana-kondoo na chochote kile kilichokuwa kizuri hawakukiangamiza. Lakini vitu vyote vibaya na visivyokuwa vya bei kali waliviangamiza.


Kwa nini basi, umezionea wivu matoleo na sadaka nilizowaamuru watu waniletee, nawe ukawaheshimu watoto wako kuliko mimi kwa kujinenepesha wenyewe kwa kula sehemu nzuri za sadaka ambazo watu wangu wa Israeli wananitolea?


Halafu Saulo akajibu: “Mimi nimefanya makosa. Rudi mwana wangu Daudi. Sitakuzuru tena kwa sababu leo maisha yangu yalikuwa ya bei kali mbele yako. Mimi nimekuwa mupumbafu na nimekosa vibaya sana.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ