Lakini Ahiya alipomusikia anaingia kwenye mulango, alisema: “Karibu ndani muke wa Yeroboamu. Lakini mbona unajigeuza kuwa mutu mwingine? Niko na ujumbe usiokuwa muzuri kwako!
Sasa musimame palepale munapokuwa kusudi mimi na ninyi tuhukumiwe mbele ya Yawe, nami nitawahutubia juu ya matendo yake ya ajabu ambayo aliyatenda kwa kuwaokoa ninyi na babu zenu.
Samweli akamwambia: “Ingawa unajiona kwamba wewe ni mudogo, lakini si wewe kiongozi wa makabila ya Israeli? Yawe alikupakaa mafuta kwa kukusimika kuwa mufalme juu ya Israeli.