1 Samweli 15:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 200211 “Ninajuta kwamba nimemufanya Saulo kuwa mufalme. Yeye ameacha kunifuata mimi na hajatimiza amri zangu.” Samweli alikasirika, akamulilia Yawe usiku kucha. အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
Lakini wakati malaika aliponyoosha mukono wake kuelekea Yerusalema kwa kuuangamiza, Yawe alibadilisha nia yake. Yawe akamwambia yule malaika aliyetimiza maangamizi kwa watu: “Basi! Inatosha; rudisha mukono wako.” Malaika wa Yawe alikuwa amesimama karibu na kiwanja cha kupepetea ngano cha Arauna wa muji wa Yebusi.
Kwa hiyo akaomba: Yawe, si hayo ndiyo mambo yaleyale niliyowaza utayafanya nilipokuwa katika inchi yangu? Ndiyo maana nilifanya haraka kukimbilia Tarsisi. Nilijua kwamba wewe ni Mungu ambaye umejaa huruma na rehema, haukasiriki upesi, wewe ni mwingi wa wema, na tayari kubadilisha nia yako kusudi usiazibu.