Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 14:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Yonatani akamwambia yule kijana aliyemubebea silaha: “Kuja, tuende kwenye ile kambi ya hawa watu wasiotahiriwa. Labda Yawe atatusaidia, maana Yawe haokoi kwa kutegemea wingi au uchache wa watu.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 14:6
31 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Musiuambie muji wa Gati jambo lile wala katika barabara za Askeloni, kusudi wanawake wa Wafilistini wasishangilie, wabinti za wapagani wasifurahi.


Labda Yawe ataangalia mateso yangu, naye atanilipa wema kwa laana hii ninayopata leo.”


Labda Yawe, Mungu wako, alisikia maneno ya yule jemadari ambaye ametumwa na bwana wake mufalme wa Asuria, kwa kumutukana Mungu Mwenye Uzima, naye Yawe, Mungu wako atamwazibu kwa ajili ya maneno aliyosikia. Uwaombee watu wanaobaki.’ ”


Hapo Asa akamulilia Yawe, Mungu wake, akisema: “Ee Yawe, hakuna mwingine kama wewe, mwenye uwezo wa kusaidia jeshi likuwe zaifu au lenye nguvu. Utusaidie, ee Yawe, Mungu wetu, kwa sababu sisi tunakutegemea wewe, na kwa jina lako tumekuja kupigana vita na jeshi hili kubwa ajabu. Ee Yawe, wewe ndiwe Mungu wetu; usimuruhusu mwanadamu yeyote ashindane nawe.”


Yawe akawashinda Waetiopia mbele ya Asa na jeshi lake la watu wa Yuda. Waetiopia wakakimbia.


Yawe anafanya chochote anachotaka, mbinguni, katika dunia, ndani ya bahari na shimo ndefu.


Anayetaka kujivuna, ajivune kwamba ananifahamu mimi, kwamba anajua kwamba mimi Yawe ninatenda mema, ninafanya mambo ya haki kufuatana na sheria yangu katika dunia. Watu wa namna hiyo ndio wanaonipendeza. –Ni ujumbe wa Yawe.


Wamisri, Wayuda, Waedomu, Waamoni, Wamoabu na wakaaji wote wa jangwa wanaonyoa nywele zote za pembenipembeni ya kichwa. Maana watu hawa wote na Waisraeli wote hawajatahiriwa mioyo yao.


Muchukie mabaya, mupende mazuri, na kudumisha sheria ya Mungu katika tribinali. Labda Yawe wa majeshi atawarehemu watu wa kabila la Yosefu waliobaki.


Mutafute Yawe, enyi wanyenyekevu wote katika inchi, enyi munaozitii amri zake. Mutafute haki, mutafute unyenyekevu; labda mutaiponyoka siku ya kasirani ya Yawe.


Yule malaika akaniambia vilevile niseme neno hili la Yawe juu ya Zerubabeli: Hauwezi kushinda kwa nguvu au kwa uwezo wako mwenyewe, lakini kwa musaada wa roho wangu. –Ni Yawe wa majeshi anayesema.


Tena ukienda nasi chochote chema Yawe atakachotutendea, ndicho utakachotendewa nawe vilevile.


Kutoka kila kabila la Israeli, mutapeleka watu elfu moja kwa vita.


Yesu akawaangalia na kuwaambia: “Jambo hilo haliwezi kutendeka kwa uwezo wa mwanadamu, lakini kwa uwezo wa Mungu, yote yanawezekana.”


Basi kufuatana na mambo hayo, tuseme nini zaidi? Mungu akiwa upande wetu, ni nani anayeweza kupingana nasi?


Mutu mumoja anaweza namna gani kuwashinda watu elfu moja, au watu wawili wanaweza namna gani kuwashinda watu elfu kumi, isipokuwa kama mulinzi wao amewatupa, Yawe amewaacha?


Sisi ndio wenye kutahiriwa kwa kweli, maana tunamwabudu Mungu kwa uongozi wa Roho wake na kujivuna kwa ajili ya Yesu Kristo. Sisi hatuweki tumaini letu katika mambo ya kimwili.


Sasa ninaomba unipe inchi hii ya milima ambayo Yawe aliniahidi siku ile. Wewe ulisikia siku ile kwamba Waanaki waliishi humo katika miji yenye kuta; labda Yawe atakuwa pamoja nami, nami nitawafukuza kama vile Yawe alivyosema.”


Kisha Samusoni akashikwa na kiu sana. Basi, akamwomba Yawe, akisema: “Ee Mungu, wewe ndiwe uliyeleta ukombozi huu, kwa kunitumia mimi mutumishi wako. Sasa utaniacha nikufe kwa kiu na kutekwa na Wafilistini hawa wasiotahiriwa?”


Chongo moja ilikuwa upande wa kaskazini wa muji wa Mikimasi na ingine ilikuwa upande wa kusini kuelekea muji wa Gibea.


Yule kijana aliyemubebea silaha akamwambia: “Fanya chochote unachotaka kufanya, mimi niko pamoja nawe maana wazo lako ndilo wazo langu.”


Daudi akawauliza wale waliokuwa karibu naye: “Mutu atakayemwua Mufilistini huyu na kuikomboa Israeli kutokana na haya hii atafanyiwa nini? Ni nani huyu Mufilistini, mutu mupagani, anayesubutu kuwatukana waaskari wa Mungu Mwenye Uzima?”


Mimi mutumishi wako nimekwisha kuua simba wengi na dubu wengi. Sasa, hata yule Mufilistini mupagani, ambaye amewatukana waaskari wa Mungu Mwenye Uzima, atakuwa kama wao.


Siku ya leo, Yawe atakutia katika mikono yangu. Nitakushinda, nitakukata kichwa chako; na miili ya waaskari wa Wafilistini nitawapa ndege na nyama wa pori. Halafu dunia nzima itajua kwamba Mungu yuko katika Israeli.


Watu wote waliokusanyika hapa leo, watajua kwamba Yawe hahitaji mikuki kwa kuwaokoa watu. Hii ni vita ya Yawe, naye atawatia ninyi wote katika mikono yetu.”


Halafu Saulo akamwambia mutu aliyemubebea silaha: “Chomoa upanga wako unichome nikufe, kusudi watu hawa wapagani wasikuje kunichoma upanga na kunichekelea.” Lakini yule aliyemubebea silaha hakusubutu kwa sababu aliogopa sana. Kwa hiyo, Saulo alitwaa upanga wake mwenyewe, na kuuangukia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ