Abeneri aliporudi Hebroni, Yoabu alimupeleka pembeni kwenye mulango sawa vile anataka kuzungumuza naye kwa siri. Hapo Yoabu akamukata Abeneri katika tumbo kwa sababu Abeneri alikuwa amemwua ndugu yake Asaeli, na Abeneri akakufa.
Vilevile vitu vyote vilivyotolewa kwa Mungu na nabii Samweli na Saulo mwana wa Kisi, na Abeneri, na Yoabu mwana wa Zeruya, vilikuwa chini ya uangalizi wa Selomiti na wandugu zake.
Saulo alipomwona Daudi akienda kupigana na yule Mufilistini Goliati, alimwuliza Abeneri, jemadari wa kundi lake: “Abeneri, huyu ni kijana wa nani?” Abeneri alijibu: “Ee Mufalme, ninaapa kwa jina lako, mimi sijui.”
Daudi akatoka, akaenda pahali Saulo alipopiga kambi. Akaona pahali ambapo Saulo alikuwa amelala. Saulo alikuwa pamoja na Abeneri mwana wa Neri, mukubwa wa waaskari, katikati ya kambi akizungukwa na waaskari wake.