Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 14:40 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

40 Kwa hiyo, Saulo akawaambia: “Ninyi wote musimame upande ule, halafu mimi na mwana wangu Yonatani tutasimama upande huu.” Wao wakajibu: “Fanya chochote unachoona kinafaa.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 14:40
6 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Watumishi wake wakamwambia: “Sisi watumishi wako, bwana wetu mufalme, tuko tayari kufanya neno lolote unaloamua.”


Mume wake Elekana, akamujibu: “Fanya unaloona linafaa. Ngojea mpaka utakapomwachisha mutoto kunyonya. Yawe afanye kiapo chako kuwa kweli.” Basi, Hana alibaki kwake, akaendelea kumulea mutoto wake mpaka alipomwachisha kunyonya.


Kisha Saulo akawaambia watu: “Twende tuwafuatilie Wafilistini usiku, tuwashambulie na kunyanganya mali zao mpaka asubui. Hatutamwacha mutu yeyote muzima.” Watu wakamwambia: “Fanya unachoona kuwa chema kwako.” Lakini kuhani akawaambia: “Kwanza tuombe shauri kwa Yawe.”


Kama vile Yawe Mwokozi wa Israeli anavyoishi, hata kama ni mwana wangu Yonatani anapaswa kuuawa.” Lakini hakuna mutu aliyesema neno.


Saulo akasema: “Ee Yawe wa Israeli, kwa nini haujanijibu mimi mutumishi wako? Ee Yawe wa Israeli, ikiwa kosa liko kwangu au kwa Yonatani mwana wangu, basi, jiwe la Urimu lionekane. Lakini ikiwa kosa hilo liko kwa watu wako Waisraeli, jiwe la Tumimu lionekane.” Yonatani na Saulo walipatikana kuwa na kosa, lakini watu walionekana hawana kosa.


Yule kijana aliyemubebea silaha akamwambia: “Fanya chochote unachotaka kufanya, mimi niko pamoja nawe maana wazo lako ndilo wazo langu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ