maana mwisho uleule unawapata wenye haki na waovu, wazuri na wabaya, wanaohesabiwa kuwa safi na wachafu, wenye kutoa sadaka na wasiotoa sadaka. Mutu muzuri ni sawa tu na mwenye zambi, na mwenye kuapa si tofauti na asiyeapa.
Siku ile, Waisraeli walisumbuliwa sana maana Saulo alikuwa amewaapiza watu akisema: “Alaaniwe mutu yeyote atakayekula chakula mbele jua kutua, na mbele sijajilipiza waadui zangu kisasi.” Kwa hiyo, siku yote, hakuna mutu aliyeonja chakula chochote.
Kwa hiyo, Saulo akawaambia: “Ninyi wote musimame upande ule, halafu mimi na mwana wangu Yonatani tutasimama upande huu.” Wao wakajibu: “Fanya chochote unachoona kinafaa.”
Wewe, haujui kwamba wakati mwana wa Yese angali anaishi katika dunia, wewe hautaweza kuwa na uhakika wa kuwa mufalme wa inchi hii? Sasa hivi kwenda umulete hapa kwangu, kwa sababu anapaswa kuuawa.”