Wakati Yawe alipowatia Waamori katika mikono ya Waisraeli, Yoshua alimwomba Yawe mbele ya Waisraeli wote, akasema: “Wewe jua, simama kimya juu ya Gibeoni, wewe mwezi, katika bonde la Ayaloni.”
Saulo aliwachagua Waisraeli elfu tatu. Kati yao, elfu mbili alikuwa nao kule Mikimasi na katika inchi ya milima ya Beteli. Elfu moja aliwaweka kule Gibea katika eneo la Benjamina. Hao aliwaweka chini ya uongozi wa mwana wake Yonatani. Watu wengine wote waliobakia, aliwarudisha, kila mutu kwake.