Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 14:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Ahiya mwana wa Ahitubu ndugu yake na Ikabodi mwana wa Finehasi mujukuu wa Eli kuhani wa Yawe katika muji wa Shilo, alikuwa ndiye aliyevaa kizibao cha kuhani. Watu hawakujua kwamba Yonatani amekwisha ondoka.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 14:3
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kila mwaka Elekana alisafiri kutoka Rama kwenda kuabudu na kumutolea Yawe wa majeshi sadaka kule Shilo. Kule, wana wawili wa Eli, Hofuni na Finehasi, walikuwa makuhani wa Yawe.


Kisha Saulo akawaambia watu: “Twende tuwafuatilie Wafilistini usiku, tuwashambulie na kunyanganya mali zao mpaka asubui. Hatutamwacha mutu yeyote muzima.” Watu wakamwambia: “Fanya unachoona kuwa chema kwako.” Lakini kuhani akawaambia: “Kwanza tuombe shauri kwa Yawe.”


Wakati ule, kijana Samweli aliendelea kumutumikia Yawe, akiwa amevaa kizibao cha kitani.


Kati ya makabila yote ya Israeli nilimuchagua Haruni na jamaa yake kuwa makuhani wangu, wanitumikie kwenye mazabahu, wafukize ubani na kuvaa kizibao mbele yangu. Nikaipatia jamaa ya babu yako sadaka zangu ambazo Waisraeli walinitolea kwa moto.


Lakini Abiatari, mumoja wa watoto wa kiume wa Ahimeleki mwana wa Ahitubu, aliponyoka akakimbilia kwa Daudi.


Naye akamwita mutoto wake Ikabodi, maana alisema: “Utukufu wa Mungu umeondolewa kwa Waisraeli”, akiwa na maana kwamba Sanduku la Agano lilikuwa limetekwa, tena baba mukwe wake na mume wake, wote walikufa.


Kwa hiyo, walituma watumishi kule Shilo, nao wakalileta Sanduku la Agano la Yawe wa majeshi ambaye anatawala juu ya makerubi. Wale wana wawili wa Eli, Hofuni na Finehasi walikuja pamoja na lile Sanduku la Agano la Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ