na hivyo, nimeshuka kusudi niwaokoe toka mikono ya Wamisri. Nitawatoa katika inchi na kuwapeleka katika inchi nzuri na kubwa, inchi inayotiririka maziwa na asali, inchi ya Wakanana, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.
Watu wa kule ulikotutoa wasiseme: ‘Yawe aliwatoa kusudi awaue katika jangwa kwa sababu hakuweza kuwaingiza katika inchi aliyowaahidi na kwa sababu aliwachukia’.
Basi, akapakua asali kwa mikono yake, akaikula akiendelea na safari yake. Aliporudi kwa wazazi wake, akawapa asali kidogo nao wakakula. Lakini hakuwaambia kwamba alitosha asali hiyo ndani ya muzoga wa simba.
Siku ile, Waisraeli walisumbuliwa sana maana Saulo alikuwa amewaapiza watu akisema: “Alaaniwe mutu yeyote atakayekula chakula mbele jua kutua, na mbele sijajilipiza waadui zangu kisasi.” Kwa hiyo, siku yote, hakuna mutu aliyeonja chakula chochote.
Ingawa watu walipofika katika pori na kukuta asali ikidondoka kila nafasi, hakuna mutu aliyesubutu kula asali hiyo kwa kuogopa kile kiapo walichoapishwa.