Kwa njia hii basi, Yawe akamwokoa mufalme Hezekia na wakaaji wa Yerusalema kutoka mukono wa Saniharibu mufalme wa Asuria, na kutoka mukono wa waadui zake wote. Akawapa maisha ya amani na wajirani zao wote.
Lakini nitawahurumia watu wa Yuda na kuwaokoa. Mimi Yawe, Mungu wao, nitawaokoa, lakini si kwa nguvu za waaskari, au pinde, au panga, au farasi au waaskari wapanda-farasi.
Yoshua akawatuma watu kutoka Yeriko kwenda muji wa Ai, unaokuwa karibu ya Beti-Aweni, upande wa mashariki wa Beteli, akawaambia: “Mwende muipeleleze inchi.” Nao wakaenda na kuupeleleza muji wa Ai.
Kila mara Yawe alipowapelekea mwamuzi, yeye mwenyewe alikuwa pamoja na mwamuzi yule, akawaokoa toka katika mikono ya waadui zao muda wote wa maisha ya mwamuzi yule. Ingawa hivyo, Yawe aliwaonea huruma aliposikia kilio chao kutokana na mateso na masumbuko yao.
Lakini leo hii mumenikataa mimi Mungu wenu ambaye ninawaokoa kutoka hasara na huzuni zenu, nanyi mumesema: ‘Hapana! Utuwekee mufalme juu yetu.’ Sasa basi, mujikusanye wote mbele yangu mukiwa katika makabila yenu na kwa maelfu yenu.”
Wafilistini walikuwa na magari elfu makumi tatu, waaskari elfu sita wapanda-farasi na kikundi cha waaskari wa miguu wengi kama muchanga wa bahari. Wote walipanda juu na kupiga kambi yao kule Mikimasi, upande wa mashariki wa Beti-Aweni.
“Kesho, wakati kama huu, nitakuletea mutu kutoka inchi ya kabila la Benjamina, nawe utamupakaa mafuta kuwa mutawala wa watu wangu Waisraeli. Yeye atawaokoa watu wangu kutoka kwa Wafilistini, maana nimeyaona mateso ya watu wangu na kilio chao kimenifikia.”