Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 14:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Wapelelezi wa Saulo kule Gibea katika inchi ya Benjamina waliwaona watu wengi wakikimbia huku na huko.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 14:16
8 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ee Mungu, uvunje meno yao, uongoe, ee Yawe, meno ya simba wakali hao.


Mungu asimame sasa, na waadui zake watawanyike! Wanaomuchukia wakimbie mbali naye!


Mimi nitawachonganisha Wamisri wao kwa wao. Ndugu atapigana na ndugu yake, jirani atapigana na jirani yake, muji mumoja na muji mwingine, mufalme mumoja na mufalme mwingine.


Watu wa Gideoni walipopiga baragumu zao mia tatu, Yawe akawafanya Wamidiani waanze kuuana wao kwa wao katika kambi. Waliobaki wakatoroka mpaka Zerera, wakafika Beti-Sita, hata kwenye mupaka wa Abeli-Mehola karibu na Tabati.


Kulikuwa hofu kubwa katika kambi ya Wafilistini. Wote walianza kufazaika: waaskari katika kambi, watu katika mashamba kwenye kambi, hata na washambulizi. Inchi ilitetemeka. Hofu ilikuwa kubwa sana.


Saulo akawaambia watu waliokuwa pamoja naye: “Basi mujihesabu kwa kujua ni nani waliotutoroka.” Walipojihesabu, waligundua kwamba Yonatani na kijana aliyemubebea silaha walikuwa hawapo.


Hivyo, Saulo na watu wake wakajipanga na kuingia katika vita na Wafilistini. Lakini Wafilistini walianza kushambuliana wenyewe kwa wenyewe kwa muvurugiko mukubwa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ