1 Samweli 14:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
14 Katika mashambulizi hayo ya kwanza, Yonatani akiwa pamoja na kijana wake aliyemubebea silaha, aliwaua watu yapata makumi mbili katika eneo kidogo tu.
Hata sasa amekwisha kujificha katika pango moja au nafasi ingine. Ikiwa tu katika mashambulizi ya mwanzo kunakufa watu kati yetu, habari itasambaa kwamba wafuasi wa Abusaloma wameshindwa vibaya.
Basi, Yonatani akapanda akitembea kwa miguu na mikono, na yule kijana akamufuata. Yonatani aliwashambulia Wafilistini akiwaangusha chini na yule kijana alifuata nyuma akiwaua.
Kulikuwa hofu kubwa katika kambi ya Wafilistini. Wote walianza kufazaika: waaskari katika kambi, watu katika mashamba kwenye kambi, hata na washambulizi. Inchi ilitetemeka. Hofu ilikuwa kubwa sana.