Basi, binti nitakayemwambia atue mutungi wake wa maji anipatie maji nikunywe, naye akinipa mimi na kuwakunywesha ngamia wangu, akuwe ndiye uliyemuchagulia mutumishi wako Isaka. Jambo hilo litanionyesha kwamba umemutendea mema bwana wangu.”
Isaya akamujibu: “Hiki kitakuwa kitambulisho kwako kutoka kwa Yawe, kwamba Yawe atafanya kama alivyoahidi: Unataka kivuli kiende hatua kumi mbele au nyuma?”
Mungu akamwambia: “Hakika nitakuwa pamoja nawe. Utawatoa watu wa Israeli na kuja kuniabudu mimi Mungu juu ya mulima huu. Hicho kitakuwa kitambulisho kwamba ni mimi Mungu niliyekutuma wewe.”
Kule utasikia wanayosema, nawe utapata nguvu za kuweza kwenda kuwashambulia.” Basi, Gideoni akaenda pamoja na mutumishi wake Pura mpaka kwenye vituo vya walinda zamu wa kambi ya Wamidiani.