Wafilistini walikuwa na magari elfu makumi tatu, waaskari elfu sita wapanda-farasi na kikundi cha waaskari wa miguu wengi kama muchanga wa bahari. Wote walipanda juu na kupiga kambi yao kule Mikimasi, upande wa mashariki wa Beti-Aweni.
Siku moja, Yonatani mwana wa mufalme Saulo alimwambia kijana aliyemubebea silaha: “Kuja, tuende ngambo kwenye kambi ya Wafilistini.” Lakini Yonatani hakumwambia baba yake.